STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 3, 2013

Azam yaanika silaha zake kwa msimu wa 2013-2014

Kocha Stewart John Hall akionyesha makeke yake kwenye mazoezi

Wakali wa klabu ya Azam ambapo baadhi wa hawatakuwa kwenye kikosi cha msimu ujao akiwemo Gaucho (24)
 
KLABU ya soka ya Azama imeweka bayana kwamba haitaacha mchezaji iliyo na mkataba naye na wala haitaongeza mchezaji mwingine katika kikosi ilichonacho sasa. 
Kwa mujibu wa taarifa yake, Azam imesema kama ilivyokuwa wakati wa dirisha kubwa la usajili 2012/13 ambapo Azam  ilimuongeza George Odhiambo 'Blackberry' pekee, safari hii imepandisha twachezaji wawili wa U20, Mudathir Yahaya na golikipa Hamadi Juma Yahya Kadedi na kufunga zoezi la usajili.
Taarifa hiyo inanukuu ripoti toka kwa Kocha mkuu wa Azam Stewart Hall, kuwa hakuna sababu ya klabu kwenda nje kusajili wachezaji ambao viwango vyao havipishani na waliopo klabuni.
Mchezaji Abdulhalim Humoud amepata timu nchini Afrika ya Kusini, Abdi Kassim 'Babi' mkataba wake umekwisha kama ilivyo kwa Deogratius Munishi Dida huku Uhuru Selemani akirejeshwa Simba SC baada ya kumaliza msimu wa mkopo na Azam FC.
Wachezaji wengine wote waliosalia wanabaki klabuni na kocha mkuu amependekeza baadhi ya makinda wa Under 20 walioonesha viwango vya juu wapandishwe timu kubwa, wapewe mikataba na kisha wapelekwe kwa mkopo ili wakapate nafasi ya kucheza. Wachezaji hao ni Omary Mtaki na Kevin Friday.
Azam ambayo imemaliza ligi ikishika nafasi ya pili kwa msimu wa pili mfululizo itaanza kambi ya kujiandaa na msimu mpya hapo June 24 kwa mujibu wa ratiba ya mwalimu na baada ya kumaliza kipindi cha pre season, kikosi cha Azam kitasafiri nje ya nchi kucheza mechi za majaribio kama ilivyo kawaida yake.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Azam FC ni;

Magolikipa; Mwadili Ally, Aishi Salum na Hamad Juma Yahya

Mabeki; Himid Mao, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Samih Nuhu, Luckson Kakolaki, Aggrey Morris, Said Moradi, David Mwantika na Jockins Atudo

Viungo; Kipre Bolou, Salum Abubakar, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo, Humphrey Mieno na Mudathir Yahya

Washambuliaji; John Bocco, Gaudence Mwaikimba, Khamis Mcha, Kipre Tchetche, Brian Umony na Abdallah Seif Karihe

No comments:

Post a Comment