STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 24, 2013

Kibadeni akana kumtimua Kaseja Msimbazi

Kocha King Abdallah Kibadeni
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnmGiUBH2n-4bYq2A7G-O5Mg7eMw2R8U3g_2gTLIHmOvOciOk4zkgnhEV0ZbsJdpep3-YAmE7L8q-zXX7P9cJDnYcQoRAUfq3BK2wnYkoqAoZu9sLMdhdazbFee-dXHAlY_7VkAk1INgo/s1600/JUMA_KASEJA%5B1%5D.JPG
Kipa Juma Kaseja
KOCHA wa Simba, Abdallah Kibaden 'King', ameibuka na kukanusha vikali uvumi kwamba ni yeye ndiye aliyemtimua kipa chaguo la kwanza wa timu hiyo na Taifa Stars, Juma Kaseja baada ya kumtema katika orodha ya nyota wanaotarajia kuwamo katika kikosi chake cha msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Badala yake, Kibaden ambaye pia ni mchezaji nyota wa zamani wa 'Wekundu wa Msimbazi' aliyewahi pia kuandika rekodi kwa kuifikisha fainali ya Kombe la Shirikisho wakati akiifundisha mwaka 1993, amefichua kuwa Kaseja hakuwamo katika orodha ya wachezaji aliokabidhiwa na uongozi wa klabu yake hiyo.
Akizungumza na jana, Kibadeni, alisema wakati akikabidhiwa majina ya wachezaji wa timu hiyo ili aanze kuwanoa, jina la Kaseja halikuwamo na hivyo yeye hawezi kulirejesha kwa maamuzi yake binafsi.
"Sijamkata mimi, ila jina lake sikupewa. Hicho ndicho ninacheweza kukieleza... mambo mengine ni ya ndani ya klabu," alisema Kibaden, mshambuliaji nyota wa zamani wa timu hiyo aliyerejea kuwafundisha baada ya kuihama klabu aliyoiongoza msimu uliopita ya Kagera Sugar.
Alisema kwa sasa tayari ameshapata wachezaji 25 atakaokuwa nao katika msimu ujao wa ligi, huku akiwataja nyota wa kigeni kuwa ni wawili na wote wanatokea Uganda.
"Kikosi changu hakitazidi nyota 25, na wageni hadi leo (jana) ni kipa Abel Dhaira na beki Senkoomi (Samuel), mipango mingine ya ndani ni ya kiufundi. Mazoezi tunayoendelea nayo ni ya kawaida na wengi waliokuja kujaribiwa hawajanishawishi kuwachukua," aliongeza Kibaden.
Naye Kaseja ambaye aliwahi kusema kitambo kuwa hahofii kutemwa Simba, alisema kuwa hivi sasa anachofanya ni kuendelea kujiweka 'fiti' ili atumikie vizuri taifa kwa sababu yeye na wenzake wa kikosi cha timu ya taifa (Taifa Stars) wana kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa wanashinda katika mechi ijayo dhidi ya Uganda na kujiweka katika mazingira mazuri ya kufuzu kwa fainali zijazo za kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN).
"Jamani kuhusiana na Simba siwezi kusema lolote kwa sasa... ila maisha ni popote," alisema nahodha huyo wa Taifa Stars ambaye wiki iliyopita alishuhudiwa akiwa katika mazoezi ya timu ya vijana ya Simba B, akishauriana na kocha msaidizi wa timu hiyo, Amri Said.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage hakutaka kueleza wazi suala la Kaseja na badala yake akasema kuwa hivi sasa, suala la nani asajiliwe na nani aachwe liko katika mamlaka ya kamati yao ya ufundi inayoshirikiana na benchi lao la ufundi.
Rage alisema vigezo vya kusajili mchezaji ni muhimu zaidi kutekelezwa na makocha na kisha kamati ya utendaji itakuwa ya  mwisho kwa lengo la kutoa baraka.
 
NIPASHE

No comments:

Post a Comment