STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 24, 2013

Mzee Mandela hali yazidi kuwa tete

Mzee Mandela (kulia) akiwa na rais Jacob Zuma wakati hali yake ilipokuwa ikianza kutengemaa kabla ya kuelezwa imebadilika kiasi cha kuwa tishio
HALI ya Afya ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini na Mwanasiasa anayeheshimika duniani kote, Mzee Nelson Mandela inaelezwa kuwa tete.
Madaktari wanaomtibu Mwanaharakati huyo aliyeleta ukumbozi katika nchini ya Afrika Kusini, wamesema hali ya Mzee Mandela imekuwa siyo nzuri kwa saa 24 zilizopita na kwamba kwa sasa yu mahututi.
Habari hizo zimekuja kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ya Afrika Kusini zikisema kuwa bado Mzee Mandela ameendelea kusalia hospitalini mjini Pretoria kwa siku ya kumi na sita akitibiwa mapafu yaliyosababisha tatizo kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma alimtembelea Rais Mstaafu huyo jana jioni na kuzungumza na jopo la matatibu wanaomtibia.
Baadaye Rais Zuma alirejea kauli yake ya kulitaka taifa na dunia kumuombea Mzee Mandela apate nafuu kwa hali aliyonayo.

No comments:

Post a Comment