STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 24, 2013

Soggy Doggy Anter atangaza kuwania ubunge Jimbo la Segerea analoshikilia Makongoro Mahanga

Soggy Doggy Anter akiwajibika jukwaani

MSANII nguli wa muziki wa kizazi kipya nchini, Anselm Tryphone Ngaiza, 'Soggy Doggy Anter' ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
Soggy Doggy ameweka bayana mipango yake hiyo ha kuwania kiti cha ubuinge cha jimbo hilo kinachoshikiliwa kwa sasa na Mhe. Makongo Mahanga kupitia akaunti yake ya Facebook ambapo aliandika;
"Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
Msanii huyo alisema ameamua kujitosa kwenye siasa kupitia CHADEMA, kwa sababu ndicho chama pekee anachokiona kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwa sasa.

No comments:

Post a Comment