STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, June 24, 2013

Balotelli kuikosa Hispania Nusu Fainali ya Kombe la Mabara

Mario Balotelli 'Super Mario'
MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya taifa ya Italia 'Azzurri' Mario Balotelli, atalikosa pambano la Nusu Fainali ya Kombe la Mabara dhidi ya Hispania siku ya Alhamis kutokana na kuwa majeruhi.
Balotelli aliumia na kutoka uwanjani wakati Italia ikichezea kichapo cha mabao 4-2 toka kwa Brazili Jumamosi iliyopita na kuungana na wachezaji wengine wa Azzurri watakaolikosa pambano hilo ambao ni  Andrea Pirlo na Riccardo Montolivo.
Kukosekana kwa Balotelli kunamfanya kocha wa timu hiyo ya Italia, Cesare Prandelli kuwa katika mtihani mkubwa katika pambano hilo dhidi ya Mabingwa wa Ulaya na Dunia, Hispania walioinyoa Nigeria jana usiku kwa mabao 3-0 na kumaliza mechi za makundi bila kupoteza mechi.
Mshambuliaji huyo mtukutu mwenye umri wa miaka 22 na anayeichezea AC Milan katika michuano hiyo amefunga mabao mawili mpaka sasa. na atakosa fursa ya kuisaidia timu yake iliyokumbana na kipigo cha aibu katika Fainali ya Kombe la Ulaya Euro Cup 2012 pale Hispania walipowanyoa kwa mabao 4-0.
Nusu Fainali nyingine ya michuano hiyo itachezwa keshokutwa kati ya Brazil ya Neymer na Uruaguay ya Luis Suarez ambao usiku wa kuamkia leo walitoa kipigo cha mabao 8-0 kwa Tahiti iliyoweka rekodi ya kushiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza ikifungwa mechi zote tatu za makundi na kufunga bao moja tu huku yenyewe ikiruhusu jumla ya mabao 24.

No comments:

Post a Comment