STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 30, 2013

29 wafa kwa kuteketezwa kwa mlipuko wa lori la mafuta lililoanguka Uganda

Picha zote hazihusiani na ajali hiyo ya Uganda

WATU 29 wameripotiwa kufa nchini Uganda na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa vibaya na moto uliotokana na ajali ya lori la mafuta lililoanguka.
Habari kutoka Uganda zinasema ajali hiyo ya kusikitisha ilitokea katika barabara kuu ya jijini Kampala na kwamba zaidi ya pikipiki 20 nazo ziliungua kwenye tukio hilo ambalo limethibitishwa na jeshi la Polisi nchiini humo.
Inaelezwa kuwa mara lori hilo lilipoanguka wakazi wa jijini hilo walilivamia kwa nia ya kuzoa mafuta kabla ya kutokea mlipuko uliowaunguza watu hao ambao baadhi walikimbilia kwenye madimbwi ya maji ili kupoza machungu ya moto na kupotea uhai wao na kuopolewa kwenye maji.
Zaidi ya watui 2o wameripiwa kukimbizwa hospitalini wakiwa hoi kwa kujeruhiwa na moto huo ambapo unaelezwa ulianzishwa na mmoja wa wahanga hao wakati wakimbilia kwenye ajali hiyo bila kujua lori lilikuwa limerbeba petroli.

No comments:

Post a Comment