STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 24, 2013

Coastal Union yatafuna 'fupa' lililozishinda Simba, Yanga

Coastal Union
MABINGWA wa zamani wa kandanda nchini, Coastal Union ya Tanga jioni ya leo imekifanya kile kilichowashinda vigogo Simba na Yanga kwa kuidungua URA ya Uganda kwa bao 1-0.
URA iliyoikwanyua Simba kwa mabao 2-1 na kusalia kidogo kuiangusha Yanga baada ya wanajangwani hao kuchomoa jioni na kupata sare ya 2-2, waliduwazwa na wagosi wa kaya kwenye uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.
Coastal ikiwa na sura mchanganyiko katika kikosi chake inaelezwa iliwakimbiza Waganda hao kabla ya Kenneth Masumbuko kuwalaza mapema kwa bao tamu.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa pambano hilo, Coastal iliwazima kabisa wageni hao waliopo nchini kwa michezo ya klirafiki ya kimataifa kwa pasi murua za Haruna Moshi Boban, Uhuru Seleman, Jerry Santo, Caspian Odula na Daniel Lyanga.
Kikosi hicho ca Coastal ambacho0 ukuta wake ulikuwa chini ya Juma Nyosso, kipo katika maandalizi ya Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Agosti 24 ambapo yenyewe itaanzia ugenini dhidi ya maafande wa JKT Oljoro.

No comments:

Post a Comment