STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 24, 2013

Taifa Stars kuifuata Uganda the Cranes leo

Vijana wa taifa Stars
TIMU ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajiwa kuondoka mchana wa leo ikitokea Mwanza kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilikuwa kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itakayocheza fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Stars itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.
Stars inahitaji ushindi wa mabao yasiyopungua mawili ili kusonga mbele kwenye fainali hizo baada ya kupoteza ya kwanza iliyochezwa nyumbani wiki mbili zilizopita kwa kufungwa bao 1-0.
Kocha wa timu hiyo jana alizungumza na wanahabari jijini humo na kutamba kwamba vijana wake wapo tayari kwa pambano hilo la Jumamosi na kuahidi watafia uwanjani, mradi kuipa nafasi Stars kurejea ilichokifanya mwaka 2009 iliposhiriki fainali hizo za CHAN zilipofanyika Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment