STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 24, 2013

Miaka 13 ya Jide kuhamia Arusha wakati wa Idd el Fitri

Lady Jaydee

MWANADADA mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura Mbibo 'Lady Jaydee' a.k.a Anaconda, anatarajia kuendeleza shamrashamra za maadhimisho ya miaka 13 ya uwepo wake kwenye fani hiyo katika mkoa wa Arusha wakati wa sikukuu ya Idd el Fitri.

Kwa mujibu wa Meneja wa msanii huyo, Gadna G. Habash maonyesho hayo yafanyika kwa siku mbili mfululizo kuanzia Idd Mosi na Idd Pili na atashirikiana na wasanii kadhaa wakongwe akiwamo Joseph Haule 'Profesa Jay wa Mitulinga a.k.a Big Daddy ambaye ni mkongwe mwenzake katika tasnia hiyo nchini.

Onyesho la kwanza la Binti Machozi litafanyika kwenye ukumbi wa  'Triple A' siku ya Idd Mosi na siku inayofuata atawapa shangwe wakazi wa jiji hilo katika ukumbi wa Botaniko Garden ambapo shughuli nzima ya burudani itaanza majira ya mchana kwa kushirikisha watoto kuonyesha vipaji vyao.

Watoto haao watashindana kucheza, kuimba na vipaji vingine mradi nao kujumuika na Anaconda kabla ya kuwapisha wazee wao kuadhimisha miaka hiyo 13 na mkali huyo asiye na mpinzani nchini miongoni mwa wasanii wa kike.

Hayo yatakuwa maadhimisho ya pili kwa Jide baada ya awali kufanya kama hivyo jijini Dar es Salaam Juni 14 ambapo alifunika mbaya kiasi kwamba ukumbi haukutosha kwa jinsi ulivyofurika watu waliojitokeza Nyumbani Lounge.

Mara baada ya maadhimisho hayo ya Arusha, Jide anatarajiwa kufanya ziara mikoa mbalimbali ili kuwapelekea burudani mashabiki wake katika kuadhimisha miaka hiyo 13 ambapo mwanamuziki huyo amekuwa akizifanya shughuli za muziki bila kutetereka akitajwa kama mmoja wa wanamuziki matarajiri Afrika Mashariki, lakini asiye na makeke.

Katika mipindi chote cha miaka 13 katika ulimwengu wa muziki, Jide ameshatoa albamu sita ambazo ni Machozi (2000), Binti (2003), Moto (2005), Shukrani (2007), The Best of Lady Jay dee(2012) na ya sasa ya Nothing but the Truth akiwa pia anamiliki bendi ya Machozi, Hoteli na miradi mingine ya kiuchumi.

No comments:

Post a Comment