STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 24, 2013

Liverpool bado yaidengulia Arsenal juu ya Suarez

Suarez

LONDON, Uingereza
LIVERPOOL imekataa ofa iliyoboreshwa ya Arsenal ya paundi milioni 40 kwa ajili ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Uruguay, Luis Suarez.

Ofa hiyo isiyo ya kawaida, inayofahamika kuwa ni paundi 40,000,001, iliandaliwa maalum kuvuka kidogo bei ya kipengele cha kuvunjia mkataba wa mchezaji huyo, lakini Liverpool wamekataa.

Chini ya vipengele vya mkataba wa Suarez, klabu hiyo inabanwa kutafakari ofa yoyote kwa ajili yake inayozidi paundi milioni 40 na ni lazima imfahamishe mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 kuhusu ofa hiyo.

Lakini Liverpool hawataki kumuuza na sasa wamekataa ofa mbili kutoka Arsenal. Ofa ya kwanza ilikuwa ni paundi milioni 30.

No comments:

Post a Comment