STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 29, 2013

Polisi Dar wachimba mkwara mzito kuelekea sikukuu ya Eid

http://www.ippmedia.com/media/picture/large/Kova1(3)(2)(3).jpg
Kamanda Kova
JESHI la Polisi Kanda Maalum Mkoa wa Dar es Salaam imewatahadharisha na kuwaonya wakazi wa jiji hilo kuhusiana na vitendo vya uhalifu wakati wa kuelekea sikukuu ya Idd el Fitri ikiwataka kuwafichua wahalifu wanaoishi nao kabla kuingia matatani wahalifu hao watakapokamatwa.
Aidha jeshi hilo limesema limejipanga vyema katika kukabiliana na vitendo vyovyote vya uhalifu kwa kupeana mbinu mpya na kuwataka wakazi wa jiji hilo la Dar es Salaam kutokuwa na hofu yoyote na kuwahimisha wafanyabiashara kufanya shughuli zao kwa amani na utulivu bila mchecheto.
Kamanda wa Polisi kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema jeshi lao limejipanga vyema kukabiliana na vitendo vyote vya uhalifu kuelekea katika sikukuu na wakati wa sikukuu yenyewe, lakini akasema wanawategemea ushirikiano wa wananchi kwa kuwafichua wahalifu hao mahali walipo.
Kamanda Kova, alisema kwa vile wahalifu wanaishi katika nyumba za wakazi hao, ni wajibu wao kuwafichua wahalifu au watu wanaowatilia shaka ili Polisi lifanye kazi zake na ikitokea wahalifu hao wakaachwa hadi waje wakamatwe basi wahusika wa nyumba au eneo hilo wataingizwa matatani.
"Kama wananchi wanajua mahali walipo wahalifu au wanaishi nao na kushindwa kuwafichua siku tukiwatia mikononi watambue wenye nyumba hiyo nayo wataunganishwa pamoja na wahalifu hao, hivyo tunawatahadharisha na kuwaomba raia wema wasifumbie macho uhalifu," alisema Kova.
Aliongeza, Polisi wamejipanga kukabiliana na vitendo vyote vya uhalifu na hasa uvamizi wa kwenye maeneo ya biashara katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye sikukuu, lakini pia wanajitaji msaada na ushirikiano mkubwa toka kwa raia wema kudhibiti vitendo hivyo.
Kadhalika aliwatoa hofu wafanyabiashara na wateja wao kuwa wafanye shughuli zao kwa amani na utulivu kwa vile Polisi wamejipanga na kutawanya vijana wao kila mahali kuhakikisha jiji la Dar es Salaam na raia wake wanakuwa katika hali ya utulivu na salama.
Kamanda Kova alisema jeshi la Polisi linajisikia vibaya kuona raia wake wakiishi kwa wasiwasi mkubwa wa matendo ya uhalifu na hasa mtindo mpya wa kihalifu uliozuka hivi  karibuni wa kutumia pikipiki na kwamba wamehamasishana na kupeana mbinu mpya kukabili vitendo hivyo.
Kova aliyasema hayo mapema leo asubuhi wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Kumepambazuka cha Radio One Stereo.

No comments:

Post a Comment