STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 29, 2013

Golden Bush Fc yatinga 10 Bora ligi ya Kinondoni


Kikosi cha Golden Bush Fc wakiwa na  makocha wao (wa kwanza kushoto waliosimama)  ni Waziri Mahadh 'Mandieta' na wa nane toka kushoto waliosimama) ni Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio'
TIMU ya soka ya Golden Bush Fc ya Sinza imekuwa klabu ya kwanza kufuzu hatua ya 10 Bora ya Ligi ya TFF Wilaya ya Kinondoni kuwania kupanda Daraja la Tatu baada ya kuikwanyua Spallows ya Kijitonyama kwa mabao 2-0.
Katika pambano hilo lililochezwa jana kwenye uwanja wa Mwananyamala, jijini Dar Es Salaam Golden Bush inayonolewa na nyota wa zamani wa Tanzania Shija Katina, Madaraka Seleman na Waziri Mahadh, ilipata mabao yote kupitia Zola.
Ushindi huo umeifanya timu hiyo kufikisha jumla ya pointi 21 na kuongoza katika kundi lake na hivyo kufuzu moja kwa moja kwenye 10 Bora kusubiri timu nyingine zitakaoungana nazo kusaka nafasi tatu za kupanda daraja la tatu.
Katika mechi zake 8 ilizocheza timu hiyo mpya kabisa, imeshinda mechi saba na kupoteza moja dhidi ya Kijitonyama ambapo ilifungwa bao 1-0 na kutibua rekodi yao ya kushinda mechi mfululizo tangu kuanza kwa ligi hiyo.
Mlezi wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' amewapongeza vijana wake pamoja na benchi nzima la ufundi kwa kazi nzuri waliofanya na kuwataka wasibweteke kwa vile hatua waliyotinga ni ngumu zaidi hivyo wagang'amale ili kuweza kutimiza malengo yao ya kuja kucheza Ligi Kuu misimu michache ijayo.

No comments:

Post a Comment