STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 29, 2013

King Majuto, Mboto watikisa tena, After Death ya Kanumba kesho


MCHEKESHAJI mkongwe nchini, Amri Athuman 'King Majuto' ameibuka tena na filamu iitwayo 'Tikisa' ambayo inaendelea kutikisa katika soko la filamu Tanzania.
Katika filamu hiyo iliyoandaliwa na Salma Jabu 'Nisha' na kuandikwa na kuongozwa na Leah Richard 'Lamata', King Majuto kama kawaida yake anavunja mbavu mwanzo mwisho akishirikiana na Haji Salum 'Mboto' na wakali wengine walioigiza pamoja.
Kwa mujibu wa Lamata, mbali na  Majuto na Mboto, filamu hiyo imewashirikisha pia Hemed Suleiman 'PHD', Chuchu Hans, Jacklyne Wolper na wengine.
"Ni bonge la filamu ambalo karibu waigizaji wote wametikisa kama lilivyo jina la filamu yenyewe, ni moja ya kazi nzuri nilizowahi kuziandika na kuziongoza baada ya kutoka na 'Poor Minds' na 'Pain Killer'," alisema Lamata.
Katika hatua nyingine Lamata alisema kuwa filamu maalum ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba 'The Great Pioneer' itaachiwa rasmi mtaani kesho Jumanne na kuwataka mashabiki wa nyota huyo wa zamani aliyefariki mwaka mwaka kukaa mkao wa kula kuipata filamu hiyo.
Lamata alisema filamu hiyo iliyowashirikisha nyota lukuki waliowahi kuigiza kazi mbalimbali na Kanumba enzi za uhai wake, imetungwa na na kuandaliwa na Jacklyne Wolper Massawe na kuongozwa na yeye na kwamba baadhi ya washiriki hao ni watoto Patrick na Jennifer walioibuliwa na Kanumba kupitia filamu kama Uncle JJ, Thisi is It na nyingine.
Pia wapo akina Patcho Mwamba, Wolper mwenyewe, Ben Blanco, Stanley Msungu, Irene Paul, Shamsa Ford, Mwanaidi Suka 'Mainda', Salama Salimin 'Sandra' na wakali wengine huku mhusika mkuu akiwa ni Philemon Lutwazi 'Uncle D' ambaye ameshabihiana na marehemu Kanumba.
'Shangazi mtu' Wolper akiwa na Jennifa na Patrick

No comments:

Post a Comment