STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, July 3, 2013

Kesi dhidi ya maafisa wa Chadema yatupiliwa mbali

Mwita Waitara

KWA mara nyingine Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Singida, ilitupilia mbali kesi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyokuwa ikiwakabili, Mwita Waitara, Afisa sera na utafiti Makao Makuu na Mshauri wa Chama hicho Dk Kitila Mkumbo,

Kesi hiyo ilitupiliwa mbali baada ya Mashahidi wa Serikali kushindwa kuthibitisha aina ya matusi yaliyodaiwa kutolewa na washitakiwa, waliyomtukana Naibu Katibu Mkuu, Mwigulu Mchemba, yaliyodaiwa kutolewa na Washitakiwa.

Sababu nyingine ya kutupilia mbali kesi hiyo ilielezwa kuwa ni upande wa serikali walishindwa kumleta shahidi muhimu katika kesi hiyo Nchemba, aliyedaiwa kutukanwa ili athibitishe kwamba yeye ndiye aliyetukanwa na namna ambavyo matusi hayo yalimuathiri.

“Washatakiwa hawana kesi ya kujibu kwa kuwa mashahidi wa serikali wameshindwa kuthibitisha aina ya matusi yaliyodaiwa kutolewa na washtakiwa”.alisema Masham Hakimu wa Mahakama hiyo.

“Upande wa serikali walishindwa kumleta shahidi muhimu katika kesi hiyo Mwigulu Nchemba aliyedaiwa kutukanwa ili athibitishe kwamba yeye ndiye aliyetukanwa na namna ambavyo matusi hayo yamemuathiri”.alisema Hakimu.

Alisema, Kushindwa kwa Nchemba kufika mahakamani ni kuonyesha kwamba ama hajui kwamba alitukanwa au hakuona kosa lolote alilotendewa na hivyo Mahakama haiwezi kutoa uamuzi kwa mambo ya kuhisiwa, alisema hakimu huyo.

Awali Washtakiwa hao, walidaiwa kutenda kosa hilo Julai 14, mwaka jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Ndago wilayani Iramba, ambapo Chadema kilikuwa na mkutano wa hadhara.

Wakati ikisomwa hukumu hiyo, alikuwepo Wakili wa Washitakiwa, Tundu Lisu, ambapo Hakimu Masham alisema washatakiwa hawana kesi ya kujibu kwa kuwa mashahidi wa serikali walishindwa kuthibitisha aina ya matusi yaliyodaiwa kutolewa na washitakiwa.

Kesi hiyo ambayo imekuwa ikisuasua mara nyingi kwa upande wa serikali kushindwa kuleta mashahidi mahakamani na kusababisha kesi hiyo kuahirishwa mara kwa mara, iliibua minong’ono jambo ambalo imedaiwa lilikuwa likimkera Hakimu wa kesi hiyo.

Wadau wa mambo ya kisheria wamekuwa wakihoji maswali mengi yasiyokuwa na majibu kwamba, inakuwaje baadhi ya viongozi wa Chama tawala wanawashaiwishi watu kufungua kesi zenye maslahi yao binfasi halafu siku ya kesi hawafiki? Je ni njia ya kuwasumbua watu au ni kuwapuuza Mahakimu?

Wengi wao wamekuwa wakiwatafsiri kuwa wanafanya hivyo wakijua wao ni chama tawala hivyo wanafanya ili kuwakomoa na kuwapa usumbufu wanaotuhumiwa kwa maana ya kuwafanya wazibe midomo ya kuwatetea wananchi?

Mwananchi ambaye alikuwepo mahakamani hapo na yeye akiwa na kesi alisema, anawashauri mahakimu wakate kudharauliwa na Viongozi wa Sampuli hizo, amabo wanawashikiza watu wafungue kesi kwa kulinda heshima zao, halafu wahusika hawafiki mahakani.

Amedai, kwanza kitendo hicho kinawadharirisha wananchi ambao wanabebwa kama debe tupu likisubiri hewa liwekwe kitu, ambapo wahusika wanaoona kesi zinawaendea kombo wanajificha na hivyo kuwaacha wao kama chama wakiadhrika.

Mama ambaye alikuwa mahakani hapo akiwa na kesi ya Miradhi alisema, tabia inayofanywa na viongozi hao, inachezea muda na fedha ambayo ni kodi ya wananchi, lakini akadai badala ya Mahakimu hao kufanya kazi ya kusikiliza kesi za wananchi zenye msingi wa kuwasaidia, wanapoteza muda kwa mambo yasiyo na maana.

Aidha Mwanaharakati aliyeomba asitajwe alisema, baadhi ya Viongozi na Watanzania wasipofuta mawazo ya kufanywa watumwa Punda au Ng’ombe, baadhi ya wanasisa watawachezea hivyo wasikubali kuwafanya vihongwe, huo wao wakijificha kwenye mapambano mfano kesi hizo.

No comments:

Post a Comment