STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 25, 2013

CHAMIJATA chatembeza bakuli kusaka Mil 40

Mwenyekiti wa CHAMIJATA, Mohammed Kazingumbe
CHAMA Cha Michezo ya Jadi Tanzania (CHAMIJATA) kimewaomba wadau wa michezo kujitokeza kukisaidia chama hicho shilingi milioni 40 ili kufanikisha mashindano ya Taifa ambayo yanatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 20 hadi 24 mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CHAMIJATA Mohamed Kazingumbe wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam.
Alisema mashindano hayo ambayo yatashirikisha mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani ni moja ya utaratibu wa chama hicho kufanya michezo ya jadi kila mwaka kwa lengo la kukuza tamaduni za nchi.
Kazingumbe alisema katika mashindano hayo wanatarajia kuwa kutakuwa na michezo mbalimbali kama bao, kurusha mshale, mdako, mirela, kukuna nazi na mingine mingi ambayo itakuwa ikitambulisha michezo ya jadi nchini.
“Tunatarajia kufanya mashindo ya michezo ya jadi ya Taifa kuanzia Septemba 20 hadi 24 ila mpaka sasa changamoto kubwa ambayo inatukabili ni fedha hivyo tunaomba wadau wenye kupenda michezo hii wajitokeze kusaidia,” alisema.
Alisema hadi sasa ni mikoa michache imethibitisha kushiriki ambayo ni Pwani, Simiyu, Lindi, Morogoro, Dar es Salaam pamoja na baadhi ya taasisi za Serikali ila bado mikoa mingine inaendelea kuonyesha nia ya kushiriki.
Mwenyekiti huyo alisema mikoa ambayo bado haijathibitisha kushiriki inatakiwa kufanya hivyo hadi ifikapo Agosti 30 mwaka huu ambapo maandalizi mengine yatakuwa yanendelea.
Kazingumbe alisisitiza kwa vyama vya mikoa na wilaya kuhakikisha kuwa vinafanya mandalizi ya kutosha ili kuhakikisha kuwa ushindani unakuwa mkubwa na kuleta tija.
Aidha alivitaja vyama vya michezo ya jadi na mikoa kuhakikisha kuwa wanashirikiana ili kufanikisha mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment