STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 25, 2013

Golden Bush Veterani, Mwanza United Veterani ngoma droo


Golden Bush Veterani
 TIMU za Golden Bush Veterani na Mwanza United zimeshindwa kutambiana leo baada ya kutoshana nguvu na kutoka sare ya mabao 4-4 katika pambano kali la kusisimua lililochezwa kwenye uwanja wa Kinesi.
Mwanza United Veterani iliyosheheni wakali kama Henry Joseph, George Masatu, Aaron Nyanda, Albert Sengo, Bakari Malima na wengine walidhihirisha kuwa hawakuja Dar kushangaa 'maghorofa' kwa kuweza kuwabana wapinzani wao wanaosifika kwa kutoa vipigo kwa timu wanazocheza nao.
Katika mechi hiyo ya leo, wageni walipata mabao yao kupitia kwa Henry Joseph na Aaron Nyanda waliofunga mabao mawili kila mmoja, huku wenyeji wakipachika yao kupitia Shija Katina aliyefunga mawili, Rashid Ziada 'KR Mullah' na Abuu Ntiro waliotupia kila mmoja bao moja na kufanya hadi mwisho matokeo yawe mabao 4-4.
Uongozi wa Golden Bush umesema baada ya mechi hiyo wanajiandaa kwa pambano jingine kali siku ya Jumapili dhidi ya timu ya TASWA Fc.

No comments:

Post a Comment