STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 30, 2013

David Mwantika amrithi Kelvin Yondani Taifa Stars, kocha Kim Poulsen amuita kikosini

Beki David Mwantika (kulia) aliyeitwa Taifa Stars kuchukua nafasi ya Kelvin Yondani
Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ameongeza kwenye kikosi chake beki wa Azam, David Mwantika kwa ajili ya mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Gambia itakayochezwa Septemba 7 mwaka huu jijini Banjul.

Mwantika ameitwa kwenye kikosi hicho kuziba nafasi ya beki Kelvin Yondani ambaye ni majeruhi. 

Mbali na Yondani Stars ina wachezaji majeruhi watatu ambao kocha Kim amewaondoa kwenye kikosi hicho ni waweze kushughulikia matibabu yao. 

Wachezaji hao ni Athuman Idd 'Chuji' , Shomari Kapombe na John Bocco 'Adebayor'.

Taifa Stars imeingia kambini jana (Agosti 29 mwaka huu) na imeanza mazoezi leo jioni kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume. 

Timu hiyo inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager pia itakuwa ikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment