STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 30, 2013

Diamond nouma, amzawadia Mzee Gurumo gari...wengine mpo...!

Msanii mkongwe wa muziki wa dansi, Muhidin Gurumo akijaribu gari dogo alilokabidhiwa na mwanamuziki wa bongo fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond ‘ kutokana na kutambua mchango wake baada ya kustaafu kazi ya muziki.
Show.
Muhidin Gurumo akipokea funguo ya gari kutoka kwa Diamond
Gari alilozawadiwa mzee Gurumo.

STAA wa nyimbo za 'Kesho', 'Nataka Kulewa', 'Mawazo' na vingine, Naseeb Abdul ameonyesha mfano kwa wadau wa muziki nchini baada ya kumzawadiwa gari mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi aliyetangaza kustaafu, Muhidini Gurumo.
Diamond alimkabidhi Gurumo gari hilo kuonyesha kujali na kuthamini mchango wa mwanamuziki huyo, baada ya hivi karibuni kunukuliwa 'akilia' kwamba kwa miaka zaidi ya 50 ya kuwa mwanamuziki anastaafu akiwa hana hata baiskeli.
Alichokifanya Diamond ni jambo la kupongezwa na kuigwa na wadau wengine wa muziki kama alivyowahi kunukuliwa mwenyewe (Gurumo) kwamba angependa ale jasho na kupewa pongezi zake angali hai badala ya watu kumsubiri afe ndipo watu wajitokeze kumwagia sifa na kujifanya kumuenzi wakati akiwa hao walimtelekeza.
MICHARAZO inakupa pongezi Diamond na tunawaomba wengine wamsadie mkongwe huyo ambaye amestaafu siyo kwa sababu ya kuishiwa kimuziki, bali hali yake ya kiafya akisumbuliwa na maradhi na wenye kutaka kumchangia watume fedha kwa njia ya TiGO Pesa katika simu yake ya mkononi 0655-401383.

No comments:

Post a Comment