STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 29, 2013

Frank Ribery ndiye Mchezaji Bora Barani Ulaya awabwaga Messi na Ronaldo

Frank Ribery ambaye kiimani ni Muislam akiomba dua kabla ya kuanza pambano la soka la timu yake ya Bayern Munich

NYOTA wa Kifaransa anayeichezea klabu ya Bayern Munich, Frank Ribery amewagaragaza wakali wa Hispania, Lionel Messi wa Barcelona na Cristiano Ronaldo kwa kunyakua tuzo ya Mchezaji Bora wa Ulaya 2012-2013.
Mkali huyo aliyeisaidia Bayern Munich kunyakua taji la Ligi ya Mabingwa ya Ulaya na mengine mawili ya Ligi ya Ujerumani alitangazwa kunyakua tuzo hiyo leo barani humo.
Ribery amenyakua tuzo hiyo akimpokea Iniesta wa Barcelona aliyenyakua msimu uliopita akitanguliwa na Messi aliyetwaa mwaka 2010-2011.
Nafasi ya pili katika kimyang'anyiro hicho ilienda kwa Messim kisha Ronaldo aliyeshina nafasi ya tatu, ingawa hjakuweza kuhudhuria sherehe hizo zilizoenda sambamba na kutangazwa kwa makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu wa 2013-2014.

No comments:

Post a Comment