STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 29, 2013

Yanga, Coastal Union wavuna Sh . Mil. 152

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj404PkGb7SiEVuMydJgAD5SUi1Dn7qkqZ-XJCGqQF3h-FdUmM4SqgP3xdez_ThTpx8JPnrFmD3GbEKygqyxzrpvY7SJWe6UDXkWzwSGti0PPt1pVV8_19cFA9PBY88prvEcTXFt_7qkmc/s640/IMG_3331.JPG
Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Coastal Union lililochezwa jana (Agosti 28 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 152,296,000.

Watazamaji 26,137 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 14 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 36,947,427.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 23,231,593.22.

Mgawo mwingine ni asilimia 15 ya uwanja sh. 18,786,827.52, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 11,272,096.51, Kamati ya Ligi sh. 11,272,096.51, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 5,636,048.26 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 4,383,593.09.

No comments:

Post a Comment