STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, August 28, 2013

Mbunge Kigamboni 'afungwa' mdomo mabomu Mbagala


Mbunge Ndungulile

Na Suleiman Msuya
WAKATI ikiwa ni siku chache baada ya Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Dk. Faustine Ndungulile kutoa kauli ya kuita Kamati halali ya kufuatilia madai ya waathirika wa mabomu ya Mbagala Jijini Dar es Salaam ni matapeli, kamati hiyo imemtaka aachane na masuala hayo.
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Steven Gimonge wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Alisema ni vema Mbunge huyo akabainisha kuwa ametumwa na nani ili kuondoa sintofahamu kwa waathirika kwani wanavyofahamu suala hilo lipo chini ya maamuzi ya Rais kwa sasa.
Gimonge alisema katika mazingira ya kusikitisha Mbunge huyo amekuwa akiombwa kuhudhuria vikao ambavyo vinahusisha waathirika lakini amekuwa hatokeo jambo ambalo ni la kusikitisha.
“Tunapenda kutumia nafasi hii kuelezea sakata la Mbagala kwani tunaona hali inaanza kuchafuliwa na baadhi ya watu jambo ambalo hatujui limetokea wapi kwani suala hilo lipo chini ya Rais,” alisema.
Mwenyekiti huyo alisema kamati hiyo inamlaani Mbunge huyo kwa kauli yake hiyo kwani inaweza kuchochea uvunjifu wa amani kati ya waathirka na Serikali.
Aidha Gimonge alitoa wito kwa wanasiasa kutotumia majukwaa ya kisiasa kutaka kupoteza haki za wananchi ambao wakuwa wakidai haki zao kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment