STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 15, 2013

Balotelli aiokoa Milan na kipigo cha ugenini

Mario Balotelli akishangilia bao

STRAIKA Mario Balotelli jana aliiokoa timu yake ya AC Milan isiaibike ugenini baada ya kufunga bao dakika za nyongeza na kuipa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Torino katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Italia Seria A.
Balotelli aliyetoka kuipeleka nchi yake kwenye michuano ya Fainali za Kombe la Dunia za mwakani, alifunga bao hilo kwa mkwaju wa penati dakika ya 90+6 na kuiepushia aibu Milan walioonekana kulala 2-1.
Kabla ya hapo Milan ilijipatia bao la kufutia machozi kupitia kwa Sulley Muntari baada ya wenyeji kutangulia kupata mabao mawili yaliyofungwa na D'Ambrosio na Cerci.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo mabingwa watetezi, Juventus wakiwa ugenini mjini Milan dhidi yasa Inter Milan waliambulia sare ya bao 1-1, huku Napoli ikipata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Atalanta, huku Fiorentina nayo ikilazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Cagliari.

No comments:

Post a Comment