STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 15, 2013

Ronaldo asaini mkataba mpya Madrid kulipwa donge nono kuliko Messi

 
KLABU ya Real Madrid imethibitisha kumalizana na nyota wao kutoka Ureno, Cristiano Ronaldo kwa kumsainisha mkataba mpya wa miaka mitano wa kuitumikia klabu hiyo.
Rais wa Madrid, Florentino Perez amethibitisha kuwa, Ronaldo ameongeza mkataba huo ambapo sasa atakuwa akilipwa mshahara wa euro mil. 17 kila mwaka.
Mshahara huo utamfanya Mreno huyo aliyewahi kutamba na Manchester United amzidi nyota wa dunia Lionel Messi wa Barca kwa euro mil. 1 na kiwango anacholipwa na klabu yake.
Kusaini kwa nyota huyo kumezima uvumi kwamba Ronaldo alikuwa njiani kutaka kuihama klabu hiyo ili kurejea England kukipiga Manchester iliyokuwa ikitajwa kutaka kumrejesha.

No comments:

Post a Comment