STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 16, 2013

Ivory Coast vs Senegal, Ghana dhidi ya Misri Top 10 WC Afrika


SHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF limetangaza ratiba ya mchujo wa mwisho kwa timu za nchi za Afrika kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia za mwakani ambapo vinara wa kandanda Afrika na wababe wa Tanzania, Ivory Coast imepangwa kuanzia nyumbani dhidi ya majirani zao Senegal.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ya CAF ni kwamba mechi za kwanza zitachezwa Oktoba 10 na zile za mwisho zitakazoa wawakilishi watano wa Afrika watakaoenda Brazil zitachezwa Novemba 14 mwaka huu.
Wakati Ivory Coast walionyakua nafasi ya kwanza katika kundi C lililokuwa na timu za Morocco, Tanzania na Gambia ikipangwa na Senegal iliyoiengua Uganda wiki iliyopita, wawakilishi wa ukanda wa CECAFA, Ethiopia yenyewe imepangwa na Nigeria na itaanza kibarua chake nyumbani mjini Addis Ababa.
Mechi nyingine itakzikutanisha Tunisia dhidi ya Cameroon, huku Burkina Faso kuumana na Algeria na Ghana watavaana na Misri.

No comments:

Post a Comment