STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 16, 2013

Kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya kuanza kesho, Moyes kuanza vipi?

Eti babu we ulikuwa unafanyaje mpaka ukatisha? Kama Moyes akimuuliza Sir Alex Ferguson

KIVUMBI cha Ligi ya Mabingwa wa Ulaya hatua ya makundi kinatarajiwa kuanza kesho, ambapo 'Mashetani Wekundu', Manchester United itaanza nyumbani dhidi ya Bayer Liverkusen ambapo mashabiki watataka kuona kocha David Moyes atavuna nini katika mechi yake ya kwanza katika michauno hiyo akiwa na Man Utd
Moyes aliyemrithi kocha mwenye mafanikio wa klabu hiyo aliyestaafu Mei mwaka huu, Sir Alex Ferguson atakuwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford, akiwa na kumbukumbu ya kukwama na Everton aliyokuwa akiinoakutinga hatua ya makundi msimu wa 2005-2006 baada ya kutolewa hatua ya mwisho wa mchujo kwa kung'olewa na Villarreal ya Hispania kwa jumla ya mabao 4-2.
Je, mbinu alizorithi toka kwa SAF zitamsaidia kuweza kufanya kweli kwenye kundi lake la A ambalo linaoonekana kuwa jepesi kulinganisha na mengine? Bila shaka ni suala la kusubiri kuona baada ya mechi hiyo ya kesho na nyingine za kundi lake lenye timu nyingine za Real Sociedad ya Hispania ambayo kesho pia itakuwa nyumbani kuialika Shakhtar Donetsk ya Ukraine.
Katika kivumbi hicho kesho pia itashuhudiwa mechi za makundi mengine matatu ya BC na Dna ratiba yake inaonyesha kuwa Galatasaray ya Uturuki itaumana na Real Madrid ambayo juzi ilimuongezea mkataba mpya nyota wake Cristiano Ronaldo na kumfanya awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani, huku ikiwa na mchezaji ghali zaidi duniani kwa usajili Gareth Bale.
Pambano jingine la kundi B kwa kesho ni København  itakayoumana na Juventus, wakati mechi za kundi C itazikutanisha timu za Benfica ya Ureno dhidi ya Anderlecht ya Ubelgiji, huku Olympiakos Piraeus ya Ugiriki ikitarajiwa kuvaana na PSG ya Ufaransa.
Mabingwa watetezi, Bayern Munich ya Ujerumani yenyewe itaanza kibarua cha kutetea taji hilo iliyotwaa Mei mwaka huu kwa kuilaza Borussia Dotmund, nyumbani kuvaana na CSKA Moskva na Viktoria Plzeň itaialika Manchester City.
Keshokutwa Jumatano, kutakuwa na mechi nyingine za makundi manne yaliyosalia ambapo ratiba kamili ni kama ifuatavyo:
Schalke 04 vs Steaua BucharestChelsea   vs Basel
Olympique Marseille vs Arsenal
Napoli   vs Borussia Dortmund 
Austria Wien vs Porto
Atlético Madrid  vs Zenit
AC Milan vs Celtic
Barcelona  vs Ajax

No comments:

Post a Comment