STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 16, 2013

Jeshi la Polisi Mbeya laonya mashabiki wa soka wenye vurugu


  RPC Mbeya, Diwani Athuman
 
JESHI la Polisi Mkoani Mbeya limewaonya mashabiki wa soka mkoani humo ambao Jumamosi walifanya vurugu kubwa na kusababisha kuutia doa mkoa huo katika medani ya soka.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo mkoani humo limewaonya mashabiki hao kuwa kama watgaendelea kufanya 'upuuzi' wao kama walivyofanya katika pambano kati ya Mbeya City na Yanga basi watakiona cha moto.
 Jeshi hilo limelaani vurugu hizo ikidai linauchafua mkoa wao na pia ni tishio kwa Mbeya kuweza kufungiwa na hivyo kuwanyima mashabiki wa kweli wa soka kushuhudia mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Taarifa rasmi ya jeshi hilo la Polisi iliyotiwa saini na ASP P Mhako kwa niaba ya RPC Diwani Athuman isome mwenyewe hapo chini;
--
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANAWATAKA MASHABIKI NA WAPENZI WA MPIRA WA MIGUU WAACHE VITENDO VYA KUFANYA VURUGU KATIKA MICHEZO ITAKAYOKUWA IKIFANYIKA KATIKA UWANJA WA KUMBUKUMBU YA SOKOINE NA MKOA KWA UJUMLA, KWANI VURUGU HIZO ZITASABABISHA MICHEZO HIYO KUHAMISHIWA SEHEMU NYINGINE NA WAPENZI KUKOSA BURUDANI  PIA WANANCHI KUKOSA KIPATO, HIVYO KUUTANGAZA MKOA WETU VIBAYA. 
 
VURUGU ZILIZOTOKEA JUMAMOSI TAREHE 14/09/2013 KWA MASHABIKI KULISHAMBULIA GARI LA VIONGOZI WA TIMU YA YANGA LILILOKUWA LIMEPAKI NJE YA UWANJA PIA KULISHAMBULIA KWA MAWE GARI LILILOKUWA LIMEBEBA WACHEZAJI WA TIMU YA YANGA NA KUHARIBU KIOO CHA MLANGO WA DEREVA NA KUFANYA MAANDAMANO AMBAYO YAMESABABISHA USUMBUFU KWA WATUMIAJI WENGINE WA BARABARA SI CHA KIUNGWANA NA KISIJIRUDIE TENA KATIKA MICHEZO MINGINE.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA HAKURIDHISHWA NA VITENDO HIVYO NA KUWATAKA MASHABIKI NA WAPENZI WA MPIRA WA MIGUU KUWABAINI NA KUWATAMBUA  WALE WOTE WATAKAOFANYA VURUGU NA KULIJULISHA JESHI LA POLISI.

AIDHA JESHI LA POLISI HALITAVUMILIA VITENDO HIVYO NA KWA YEYOTE ATAKAYE/WATAKAO BAINIKA HATUA KALI ZA KISHERIA ZITACHUKULIWA ZIDI YAKE/YAO.

Signed by:
[P.A MHAKO – ASP]
Kny: KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

No comments:

Post a Comment