STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 2, 2013

Simba wee acha tu, yaitafuna mafunzo Mrundi atupia mbili

Mshambuliaji wa Simba, Tambwe Amissi (kulia) akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Mafunzo, Jumbe Omari Jumbe katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ambapo Simba ilishinda mabao 4-3 na yeye Tambwe kutupia mabao mawili.
Hekaheka katika lango la Mafunzo. 
 Beki wa Mafunzo Ali Vuai Juma (kushoto) akichuana na mshambuliaji mpya wa Simba kutoka Burundi, Tambwe Amissi. katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Beki wa Mafunzo, Jumbe Omar Jumbe akimdhibiti mshambuliaji wa Simba, Tambwe Amissi
 Golikipa wa timu ya Mafunzo ya Unguja, Ussi Makame Ussi akiwa hana la kufanya baada ya kushindwa kuzuia kiki iliyopigwa na mshambuliaji wa Simba, Tambwe Amissi (kushoto)  na kuipatia timu yake bao la kwanza katika mchezo wa kirafiki uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. (Picha na Francis Dande)
 Golikipa wa Mafunzo, Ussi Makame Ussi akiruka bila mafanikio kujaribu kuokoa mpira uliopigwa na mshambuliaji wa Simba, Tambwe Amissi na kuhesabu bao la kwanza kwa timu yake.
Mrundi Tambwe Amissi akishangilia bao aliloifungia timu yake

No comments:

Post a Comment