STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 2, 2013

Kim Poulsen aweweseka amuita Henry Joseph Stars

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRxitDiN5RLOXCBKIEoybp3pTPr5-aNuxzD0hVSuDnoAKgoQ4f3ZtjaBRCb9TkwcKTZ5q5uGvF_TEoZnFjFk267hPssx6Q6yGFkDj2S3Z4dJfXr2LSHvtVDvfxghJGYOnSCFyliv2DoII/s320/HenryJoseph.jpg
Henry Joseph
Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amemjumuisha mchezaji Henry Joseph wa Simba kwenye kikosi chake kinachojiandaa kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Gambia itakayochezwa Septemba 7 mwaka huu jijini Banjul.

Tayari Joseph amesharipoti kwenye kambi ya timu hiyo iliyoko hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam. Taifa Stars ambayo iko chini ya udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager imeingia kambini tangu Agosti 29 mwaka huu, na leo jioni itafanya mazoezi yake kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Programu ya timu hiyo inaonesha kuwa kesho (Septemba 3 mwaka huu) itafanya mazoezi yake asubuhi na jioni kwenye uwanja huo huo wa Kumbukumbu ya Karume.

Wakati huo huo, kesho (Septemba 3 mwaka huu) saa 6 kamili mchana Kocha Kim Poulsen atakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari.

No comments:

Post a Comment