STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 1, 2013

Wabongo wawili waombewa ITC Ujerumani


Na Boniface Wambura
CHAMA cha Mpira wa Miguu cha Ujerumani (DBU) kimetuma maombi ya Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa wachezaji wawili wa Tanzania ili wajiunge na klabu mbili tofauti za nchini humo.

Maombi hayo yaliyotumwa kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni kwa ajili ya wachezaji Henry Claud Egito aliyezaliwa Desemba 31, 1984 jijini Dar es Salaam, na Dominic Johnson aliyezaliwa Agosti 14, 1991 jijini Tanga.

Wachezaji hao wanaombewa ITC kama wachezaji wa ridhaa. Egito anaombewa hati hiyo ili ajiunge na klabu ya FSV Lokomotive Dresden wakati Johnson anatakiwa na klabu na TSV 1967 Schwabbruck.

No comments:

Post a Comment