STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 1, 2013

TAHLISO nao watoa mapendekezo yao Katiba Mpya

 
Na Suleiman Msuya
WAKATI jamii ya Kitanzania ikiwa imeelekeza mitazamo, michango na mawazo juu ya aina ya Katiba ambayo wanaitaka Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO) wamependekeza kuwepo kwa haki ya kupatiwa elimu bora, haki za wanaume pamoja na kuomba suala la muungano liwe la wananchi wote kutoa maoni.
Hayo yamebainshwa na Mwenyekiti wa TAHLISO Amon Chakushemeire wakati akizungumza na MICHARAZO, ambapo alisema mapendekezo hayo yametokana baraza wa wanachama wa TAHLISO ambao walikutana  Mkoani Mbeya kwa siku mbili ambapo waliweza kujadili rasimu ya Katiba wakiwa sehemu ya baraza.
Mwenyekiti baada ya kuipitia kwa undani rasimu hiyo wajumbe waligundua mambo makuu matatu ambayo ni haki ya kupatiwa elimu, haki za wanaume na muundo wa muungano ndiyo yanahitaji kuwekwa kama mapendekezo baada ya kuona watu wengi wamekuwa wakiyajadili mambo mengine na kuyaacha.
“Unajua watu wengi waliochangia rasimu ile wameonekana kusauhau suala la haki ya kupatiwa elimu, haki za wanaume jambo ambalo linaonekana kuwa linaweza kufanya yakasahaulika na kuendelea kuleta athari kwa jamii,” alisema.
Alisema suala la elimu linahitaji kubainishwa kwenye katiba moja kwa moja ili kuhakikisha kuwa jamii inapatiwa elimu kuanzia msingi hadi mahali ambapo mfaidika ataweza kutumikia jamii.
Chakushemeire alisema suala la kuwepo kwa haki za wanaume linaonekana kama halina tija ila ukweli ni kwamba jamii ya wanaume imekuwa ikipata athari kubwa ila haina pahali pa kusemea.
Mwenyekiti huyo alisema suala la muundo wa muungano ni vema likarejeshwa kwa wananchi ili waweze kufanya maamuzi wao wenyewe na lisiwe ni suala la watu wachache.
Akizungumzia suala la TAHLISO kuhusishwa na kuwapigia kampeni baadhi ya wagombea nafasi za Urais Katibu wa TAHLISO Donati Salla alisema wao hawahusiki na mambo hayo na kuwataka wanachama wao kutotumia nembo yao kufanya mambo yao binafsi.
Salla alisema wanaotajwa kuwa walikuwa viongozi wa TAHLISO huko morogoro ni kweli kuwa ni wanachama TAHLISO ila hakutumwa na wao na ni watu wenye maslahi yao binafsi jambo ambalo wanalipinga.
Aidha alitoa angalizo kwa baadhi ya watu ambao wanajiita Taasisi ya Vijana Tanzania  (TAVITA) kuacha kuwashirikisha wanachama wa TAHLISO katika mikakkati yao ya kutumiwa na watu wenye mipango ya kugombea Urais mwaka 2015.
Alisema kundi hilo linatarajiwa kukutana Septemba 7 mwaka huu nyumbani kwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu wilayani Monduli.

No comments:

Post a Comment