STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 1, 2013

Thamani ya SAkiba ya Wafanyakazi yafikia Bil. 178

 
Na Suleiman Msuya
THAMANI ya Mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi Serikali imekuwa kutoka bilioni 72.55 mwaka 2008/2009 hadi kufikia bilioni 178.3 mwezi Juni mwaka 2013.08.30
Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa GEPF Festo Fute wakati akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Alisema ongezeko hilo limechangiwa na kuongezeka kwa wanachama pamoja na uwekezaji katika sekta mbalimbali kama amana  za serikali, makampuni yaliyo orodheshwa kwenye soko la mitaji (DSE), uwekezaji wa muda maalum kwenye mabenki ya biashara, mikopo, hati fungani na majengo.
Fute alisema hadi kufikia mwaka huu GEPF imefanikiwa kusajili wanachama 60, 030 ambapo kwa kipindi cha mwaka 2008/2009 walikuwa wanachama 30,227  hiyo ikitokana na jitihada zao za kuhakikisha kuwa watu wote wanafaidika na mfuko huo.
“Unajua katika mifuko hii ya hifadhi ya jamii moja ya malengo yake ni kuhakikisha kuwa thamani ya mfumo inaongezeka jambo ambalo tumeweza kulitekeleza kwani sasa mfumo una thamani ya shilingi bilioni 198.30,” alisema.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema vitegauchumi wa mfuko viliongezeka kutoka shilingi bilioni 64.94 mwaka 2009 hadi kufikia shilingi 179.68 mwaka 2013, ambapo na mapato yameongezeka  kutoka shilingi bilioni 5.48 mwaka 2009 hadi bilioni 18.25 mwaka 2013.
Alisema pamoja mafanikio hayo ya thamani ya mfuko ila pia wamekuwa wakiwalipa wanachama wao mafao kwa wakati ambao kwa kipindi cha mwaka 2012 hadi 2013 zaidi ya bilioni 5 zimelipwa kwa wanachama kama mafao.
Aidha akizungumzia kuhusu mpango wa hiari wa kujiwekea akiba ya uzeeni (VSRS) alisema mfuko huo umekuwa na mafanikio makubwa ambapo tangu mwaka 2009 hadi 2013 wameweza kusajili na wanachama 18,700 ambapo jumla ya akiba za wanachama zilifikia kiasi cha shilingi bilioni 3.05.
Fute alisema katika mfuko huo wanachama wamegawanyika katika makundi mbalimbali ambayo ni wafanyabiashara 7,480, kilimo ufugaji 6,545, ujasiriamali 1,683 na waajiriwa 2,992.
Pia alisema pamoja na mafanikio ambayo wameyapata pia mfumo huo unakabiliwa na changamoto mbalimbali kama kupitwa kwa sheria inayoongoza mfuko na ufahamu mdogo wa watu kuhusu mfuko.

No comments:

Post a Comment