STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 2, 2013

Liunda kutathimini waamuzi CAF

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUOM9IRMZijo63-gOG0Myp2_FetrrPAa1FMIGgam1cJJeCV3Zw9RJxhccBlTqfqv1BugkRqtKZpQeEqBNDPehsoBY_0JHLwIcpdrPLMoLPcJYFT2o3h3y1-9g6SWu_adMOBBokNV6MFCU/s1600/liunda.JPG
Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Leslie Liunda wa Tanzania kuwa mtathmini wa waamuzi kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Coton Sport ya Cameroon na Esperance ya Tunisia.

Mechi hiyo ya kundi B itachezwa Septemba 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Omnisport Roumdeadjia mjini Garoua, Cameroon. Kamishna atakuwa Bema Doumbia wa Ivory Coast.

Waamuzi wanatoka Madagascar wakiongozwa na Hamada Nampiandraza. Wasaidizi wake ni Jean Eric Pierre Andrivoavonjy, Ferdinand Velomanana Linoro na Bruno Marie Andrimiharisia.
 

No comments:

Post a Comment