STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 28, 2013

Chelsea, Spurs zang'ara, Sunderland ikiona mwezi EPL

 
UZEMBE uliofanywa na kipa Joe Hart kutoka golini bila kuwasiliana na beki wake, Nastasic aliyekuwa akimrudishia mpira kwa kichwa, uliiwezesha Chelsea kupata bao lililowapa ushindi dakika ya lala salama na kukwea hadi nafasi ya pili katika Ligi Kuu ya England.
Fernando Torres aliuwahi mpira uluioonekana kama unaelekea nje ya lango lililokuwa wazi la Man City na kuipatia timu yake bao muhimu na kushinda 2-1 kartika pambano lililokuwa kali lililochezwa uwanja wa Stamford Bridge.
Awali, Torres alitoa krosi nzuri kwa Schurrle aliyeifungia Chelsea bao la kuongoza katika dakika ya 32 lililodumu haidi mapumziko kabaal ya wageni kulirejesha dakika tatu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili kupitia kwa Sergio 'kun' Aguero.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana, Tottenham iliendelea kufukuzia nafasi za juu baada ya kuinyuka 
Hull City kwa bao 1-0 lililofungwa na Roberto Saldado, nao wachovu wa ligi hiyo Sunderland waliwafunga wapinzani wao Newcastle United kwa mabao 2-1 ikiwa ndiyo ushindi wao wa kwanza msimu huu na timu za Swansea City na West Ham wakitoshana nguvu kwa kutoka 0-0.

No comments:

Post a Comment