STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 28, 2013

Maskini Wema Sepetu! Afiwa na baba yake mzazi

STAA wa filamu na aliyewahi kuwa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu amepatwa na msiba mzito baada ya baba yake mzazi Balozi Issac Abraham  Sepetu kufariki dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya TMJ Mikocheni jijini.
Inaelezwa kuwa, Balozi Sepetu alikuwa amelazwa katika hospital ya TMJ akitibiwa ugonjwa wa Kisukari na kiharusi uliokuwa ukimsumbua kwa muda mrefu sasa.
Hadi umauti unamkuta, Balozi Isaac Sepetu alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar na taarifa zilizopo ni kwamba anatarajiwa kuzikwa visiwani Zanzibar siku ya kesho.
Mtandao huu wa MICHARAZO MITUPU unaungana na Wema waombolezaji wote kumpa pole Wema Sepetu na familia nzima, ndugu na jamaa wa marehemu Balozi Zepetu na kuwaomba kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu kwa kukumbuka kuwa 'Sisi ni wa Mungu na kwake tutarejea. Mwenyezi Mungu, Aiweke Roho ya Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu, Mahala Pema Peponi. Ameen

No comments:

Post a Comment