STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 28, 2013

Mwanajeshi mwingine wa Tanzania auwawa DR Congo, ashambuliwa na Waasi wa M23

Mwanajeshi anayedaiwa kuuwawa DR Congo
WATANZANIA wameendelea kupoteza ndugu zao wanaolinda amani katika mataifa ya nje baada ya taarifa za kwenye mtandao kueleza mwanajeshi aliyekuwa akihudumu katika Jeshi la Kulinda Amani MANUSCO huko DR Congo kuuwawa na waasi wa M23.
Taarifa hizo zinamtaja mwanajeshi huyo kuwa ni Rajab Ahmad Mlima aliyeshambuliwa kwa risasi wakati akijaribu kuwalinda wakazi wa mji wa Kiwanja na Ratshruru Kaskazini mwa mji wa Goma dhidi jeshi la  waasi hao wa M23.
Kifo cha mwanajeshi huyo kimekuja wakati watanzania wakiwa bado hawajasahau mashujaa wao waliouwawa Sudan Kusini na DR Congo hivi karibuni katika harakati za kulinda amani katika nchi hizo.
Mwenyezi Mung Ailaze mahali pema Peponi Roho ya mwanajeshi huyo. Ameen

No comments:

Post a Comment