STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 11, 2013

Nkongo, Chacha kuchezesha Chalenji, 18 watangazwa Tz watoa watatu tu!

BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), leo limetangaza majina ya waamuzi 18 watakaochezesha michuano ya mwaka huu ya Kombe la Chalenji itakayofanyika nchini Kenya.

Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amesema leo kuwa, kati ya waamuzi hao, tisa watakuwa wa kati na wengine tisa wasaidizi.

Musonye amesema waamuzi wote hao watalazimika kwenda Nairobi mapema kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya zao pamoja na uimara wa mwili.

Michuano hiyo imepangwa kuanza Novemba 27 mwaka huu, ikizishirikisha nchi zote wanachama wa baraza hilo kongwe barani Afrika.

Waamuzi wa kati ni :
1. Anthony Okwayo-Kenya
2. Denis Batte-Uganda
3. Wish Yabarow- Somalia
4. Israel Mujuni- Tanzania
5. Louis Hakizimana- Rwanda
6. Thiery Nkurunziza- Burundi
7. Waziri Sheha- Zanzibar
8. Gebremichael Luleseged- Eritrea
9. Kheirala Murtaz - Sudan
Waamuzi Wasaidizi ni:
1. Gilbert Cheruiyot- Kenya
2. Tonny Kidiya- Kenya
3. Mark Ssonko- Uganda
4. Fedinard Chacha- Tanzania
5. Suleiman Bashir- Somalia
6. Fraser Zakara-South Sudan
7. Simba Honore-Rwanda
8. Hamid Idam- Sudan
9. Kinfe Yimla-Ethiopia

No comments:

Post a Comment