STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 12, 2013

TANZIA! MASKINI DK MVUNGI HATUNAYE

Dk Mvungi enzi za uhai wake
Dk Mvungi alipokuwa akiipigania roho yake baada ya kujeruhiwa na majambazi
ALIYEKUWA Mjumbe wa Tume ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi amefariki dunia mchana wa leo.
Taarifa zilizotufikia kutoka Milpark Hospitali, zinasema kuwa Dk Mvungi alifariki majira ya saa 9 Alasiri alipokuwa akitibiwa baada ya kupigwa mapanga na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliomvamia nyumbani kwake Kibamba Msakuzi, Kinondoni.
Kabla ya kupelekwa Afrika Kusini, Dk Mvungi alikuwa akitibiwa katika hospitali ya Moi Muhimbili kabla ya kukimbizwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi.
Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Mwenyekiti Taifa wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Dk Mvungi ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alijeruhiwa  Novemba  3, mwaka huu.
MICHARAZO inaungana na familia, ndugu na jamaa wa marehemu Dk Mvungi katikamkipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito na kuwataka wawe na subira kwa kutambua kuwa 'KILA NAFSI ITAONJA MAUTI' Dk Mvungi katangulia sisi tuy nyuma yake. Mungu aiweke mahali pema roho ya marehemu.

No comments:

Post a Comment