STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 28, 2013

Uhai Cup 2013 yafikia patamu, nusu fainali kuanza leo Chamazi

Moja ya hekaheka za michuano ya Uhai Cup 2013
MICHUANO ya vijana kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara U20 ya Uhai Cup imeingia hatua tamu ambapo timu nne za kucheza Nusu Fainali zimefahamika na kipute hicho kinaanza leo kwa pambano la mabingwa watetezi, Azam dhidi ya Coastal Union.
Nusu fainali nyingine itachezwa kesho kwa mchezo kati ya Yanga itakayoumana na Mtibwa Sugar ambayo jana iliing'oa Simba kwa mabao 3-2, ikitoka nyuma kwa mabao 2-0.
Mechi zote hizo zinachezwa uwanja wa Chamazi, ambapo pambano la leo kati ya Azam na Coastal linarejesha kumbukumbu ya mechi mbili kwa timu hizo zilipokutana katika mechi ya Fainali za mwaka jana na Coastal kukubali kipigo kabla ya kulipa kisasi jkatika mechi ya ufunguzi wa michuano ya msimu huu walipoibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Timu hizo mbili zilifuzu hatua hiyo ya nusu fainali kwa kuzinyoa timu za maafande, Azam ikiilaza Prisons-Mbeya na Coastal kuichapa JKT Oljoro.
Mtibwa walioiduwaza Simba iliyokuwa ikipewa nafasi ya kutwaa taji hilo sawa na Ashanti United, itapepetana na Yanga ambayo imeonyesha kubadilika msimu huu tofauti na msimu uliopita, japo timu iliyowang'oa Ashanti United katika mechji yao ya robo faiali ya jana wanalalamikiwa kubebwa.
Kama Yanga itafuzu hatua hiyo itaweka rekodi kwa mara ya kwanza kufika hatua hiyo kubwa tangu michuano hiyo ilipoanzishwa mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment