STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 28, 2013

Super Nyamwela kutoka na Dully Sykes

KIONGOZI wa safu ya unenguaji wa bendi ya Extra Bongo, Hassan Mussa 'Super Nyamwela' amesema  yupo mbioni kupakua wimbo mpya atakaoimba na nyota wa muziki wa kizazi kipya, Prince Dully Sykes.
Akizungumza na MICHARAZO, Nyamwela alisema wimbo ambao hapendi kuutaja jina kwa sasa utarekodiwa katika studio za msanii huyo, ziitwazo Dhahabu Records za jijini Dar es Salaam.
Nyamwela alisema huo ni wimbo wa nne kuelekea kupakua albamu yake ya tatu baada ya awali kutoa 'Tumechete', 'Maneno' na kibao kinachoendelea kutamba kwa sasa wa 'Duvele Duvele'.
"Nipo katika maandalizi ya kuingia studio kurekodi wimbo wangu mwingine mpya ambao nitaimba na Dully Sykes, nao utakuwa kama Duvele kwa namna ya midundo yake, lengo kuwapa burudani mashabiki wangu," alisema Nyamwela.
Nyamwela alisema, anahofia kutaja jina la wimbo huo kwa sasa kwa madai ni mapema mno, pia akihofia kuibiwa 'idea' kutokana na kuwepo kwa mtindo wa baadhi ya wasanii kuiba kazi za wenzao na kuzitanguliza mapema hewani.
"Ningeutaja kwa sasa, lakini nahofia wasanii vilaza ambao hawaumizi vichwa kutoa kazi zao badala yake usubiri wasikie mawazo ya wenzao na kuwahi kutoa hewani," alisema.
Nyamwela aliyeanzia kwenye muziki wa disko kabla ya kuibngia kwenye makundi ya muziki wa dansi miaka ya 1990, aliwahi kutamba na albamu mbili za 'Master of the Tample na 'Afrika Kilomondo' alizoimba na wasanii wenye majina mkubwa nchini kama Ally Choki, Richard Maalifa na Sir Juma Nature.

No comments:

Post a Comment