STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, November 28, 2013

Vigogo' vyaua' Ulaya, Madrid, Bayern, Man U, Juve kufuru tupu!

Watetezi, Bayern Munich wakishanmgilia mabao yao
MANCHESTER City imeifumua mabao 4-2 Viktoria Plzen Uwanja wa Etihad usiku huu katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Mabao ya City yamefungwa na Aguero kwa penalti dakika ya 33, Nasri dkika ya 65, Negredo dakika ya 79 na Dzeko dakika ya 90, wakati mabao ya Viktoria Plzen yamefungwa na Horava dakika ya 43 na Tecl dakika ya 69.
MABINGWA watetezi, Bayern Munich wameendeleza wimbi lao la ushindi katika Ligi ya Mabingwa baada usiku wa kuamkia leo kuinyuka CSKA Moscow kwa mabao 3-1, huku Real Madrid ikiishindilia Galatasaray ya Uturiki mabao 4-1 na timu za Manchester zote zikipata ushindi mnono katika mechi zao.
Manchester United ikiwa ugenini nchini Ujerumani iliisasambua Bayer Leverkusen kwa mabao 5-0, huku wapinzani wao, Manchester City ikiwa nyumbani ikiicharaza Victoria Plzen kwa mabao 4-2.
Watetezi Bayern Munich waliipata ushindi wao wa 10 mfululizo na kupiku rekodi iliyowahi kuwekwa na Barcelona mwaka 2002 kwa mabao ya Arjen Robben, Mario Gotze na Thomas Muller aliyefungwa kwa penati.
Wakali wa Hispania, Real Madrid ikishuka dimbani bila nyota wake, Cristiano Ronaldo ilipata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Galatasaray licha ya kucheza pungufu baada ya Sergio Ramos akitolewa mapema kipindi cha kwanza kwa kadi nyukundu.
Winga, Gareth Bale aliwaongoza wenzake kupata ushindi huo uwanjawa nyumbani baada ya kutangulia kufunga bao la kwanza kabla ya Arbeloa kuongeza la pili katika dk ya 51, Di Maria dk ya 63 na Isco kuhitimisha karamu ya mabao dakika ya 80. Bao pekee la Waturuki lilifungwa dakika moja baada ya Bale kutangulia kuifungia Madrid, kupitia kwa Bulut.
Katika mechi nyingine Machi nyingine, Juventus ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fc Copenhagen, huku Shakhtar Donetsk ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Real Sociedad na PSG ya Ufaransa ikipata ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Olympiacos ya Ugiriki jijini Paris.
Matokeo ya mechi zote zilizochezwa jana ni kama ifuatavyo;
Kundi A
Bayer Leverksuen 0-5 Manchester United
Shakhtar Donetsk 4-0 Real Sociedad
Kundi B
Real Madrid 4-1 Galatasaray
Juventus 3-1 FC Copenhagen
Kundi C
PSG 2-1 Olympiacos
Anderlecht 2-3 Benfica
Kundi D
Manchester City 4-2 Viktoria Plzen
CSKA Moscow 1-3 Bayern Munich

No comments:

Post a Comment