STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 5, 2013

Addyng'ari awakumbuka wa nyumbani Mbeya

Addyng'ari katika pozi
MSANII anayekuja kwa kasi katika muziki wa kizazi kipya Addy Michael 'Addy Ng'ari' kutoka jijini Mbeya ameachia wimbo mpya uitwao 'Nawakumbuka Nyumbani' ambao  tayari umeanza kurushwa hewani katika vituo vya redio vya jijini humo na anafanya mchakato ili kuusambaza katika vituo vya redio jijini Dar es Salaam ili nako usikike.
Msanii huyo alisema wimbo huo ni maalum kwa wale wanaokuwa mbali na kwao na jinsi wanavyokuwa wakikumbuka nyumbani kwao kiasi kwamba hupata wakati mgumu kufanya kazi zao kwa ufanisi.
"Ni moja ya wimbo unaoelezea namna watu wanavyopata tabu wawapo mbali na nyumbani kwao  na zipo nyingine ambazo nimeshatunga na kuzifanyia mazoezi, lakini nasubiri nitoe video ya kibao hiki kabla ya kuingia tena studio," alisema Ng'ari.
Aliongeza kuwa wakati akianza mipango ya kuusambaza vituo vya redio vya jijini Dar es Salaam, pia tayari ameanza mchakato wa kuanza video yake huku akiendelea kufanyia mazoezi nyimbo nyingine mpya ili kuzirekodi.

No comments:

Post a Comment