STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 5, 2013

Man Utd hoi, Liverpool ikiua 5-1, Arsenal burudaniiii kama Chelsea

Fellaine dhidi ya timu yake ya zamani Everton na kushindwa kuitetea baada ya kulala 1-0

Natupia tu! Luis Suarez akifunga moja ya mabao yake manne usiku wa jana

Nipe tano mwanangu! Arsenal wakishangilia mabao yao walipoizamisha Hull City

Lampard akitupia kambani bao lake wakati Chelsea ikishinda mabao 4-3 ugenini
LONDON, England
WAKATI mashabiki wa Manchester United wakiendelea kupata 'vidonda vya tumbo' kutokana na timu yao kufanya vibaya, wenzao wa Arsenal wanachekaa baada ya usiku wa jana timu hiyo kuendeleza wimbi lake la ushindi.
Vijana hao wa Arsene Wenger, waliishindilia Hull City kwa mabao 2-0 na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Mabao ya Nicklas Bendtner la dakika ya pili ya mchezo na jingine la kipinbdi cha pili kupitia Mesut Ozil, lililtosha kuwafanya vijana hao wa London Kaskazini kuendelea kukenua wakati wapinzani wa Manchester United ikiendelea kununa.
Hii ni kwa sababu mabingwa watetezi hao usiku wa kuamkia leo walidunguliwa nyumbani na Everton kwa bao 1-0 lililofungwa na Bryan Oviedo baada ya mwishoni mwa wiki kulazimishwa sare ya 2-2 na Tottenham Hotspur.
Hali ikiwa hivyo, Liverpool ilitoka kufungwa mabao 3-1 ilizinduka jana kwa kuilaza Norwich City kwa mabao 5-1, huku mabao manne yakitupiwa kambani na mkali Luis Suarez na jingine likifungwa na Raheem Sterling.
Bao la kufutia machozi la Norwich liliwekwa kimiani na Johnson.
Katika michezo mingine ya ligi hiyo iliyochezwa usiku wa jana, Chelsea ilipata ushindi wa kindondokela baada ya kuzima Sunderland nyumbani kwao kwa mabao 4-3, huku wenyeji wakijifunga moja ya mabao hayo.
Chelsea ilipata ushindi huo kwa mabao ya Frank Lampard, Eden Hazard aliyefunga mawili kabla ya Bardsley kuwazadia bao wakati katika harakati za kuokoa mpira. Wenyeji walipata mabao yao ya kufutia machozi kupitia kwa  Altidore na Bardsley.
Naye Mwanasoka Bora wa Afrika wa BBC, Yaya Toure alifunga magoli mawili wakati timu yake ya Manchester City ikipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya West Brom.
Sergio Kun Aguero aliifungia City bao jingine na kuwasogeza hadi nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo, huku wapinzani wao wakipata mabao yake kupitia kwa Pantilimon na Anichebe.
Tottenham nayo ilizinduka kwa kupata ushindi wa jioni wa mabao 2-1 dhidi ya wenyejki wao Fulham waliotangulia kupata bao kupitia kwa Dejagah katika kipindi cha pili.
Spurs walipata mabao yake yaliyowafanya wajongee kwenye msimamo hadi nafasi ya sita kupitia kwa Chiriches aliyesawazishia na Holtby aliyefunga bao la ushindi.
Nayo Newcastle United baada ya kupata ushindi mfululizo jana ilijikuta ikikwama ugenini baada ya kufungwa mabao 3-0 na Swansea City, huku Aston Villa ikiwa ugenini ikipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Southampton na Stoke City ikibanwa nyumbani na Cardiff City kwa kutoka sare ya kutofungana.

No comments:

Post a Comment