STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 21, 2013

Amissi Tambwe aizamisha Yanga Taifa

Kitu Simba wakiandika bao lao la kwanza dhidi ya Yanga
Sisi ndiyo Majembe ya Ukweli tusio na longolongo nyingi

MABAO mawili ya Mrundi Amissi Tambwe na jingine la Awadh Juma yametosha kuwanyamazisha Yanga licha ya Emmanuel Okwi kufunga bao la kufutia machozi wakati Simba ikipata ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe uliomaliza hivi punde uwanja wa Taifa.
Tambwe, anayeongoza kwa magoli katika Ligi Kuu Tanzania Bara alifunga bao la kwanza dakika ya 14 kabla ya kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati dakika 43 baada ya David Luhende kumuangusha mshambuliaji aliyeichachafya Yanga kwa siku ya leo, Ramadhani Sindano 'Messi' na kuifanya Yanga kwenda mapumziki wakiwa nyumba kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili kilichokuwa na mshikemshike kilishuhudia timu zote zikipata bao moja moja , Simba wakitangulia dakika ya 62 kupitia kiungo aliyetua Simba akitokea Mtibwa Sugar,Awadh Juma  kabla ya Okwi kufunga kwa kichwa akiunganisha krosi ya Simon Msuva dakika ya 87.
Katika mechi hiyo iliyokuwa kali ilishuhudiwa beki kisiki, Kelvin Yondani akitolewa kwa kadi nyekundu baada ya kuonyesha kadi mbili za njano baada ya kumuangusha Ramadhani Singano 'Messi'.
Langoni mwa Yanga lidaka kipa wa zamani wa Simba, Juma Kaseja ambaye kipigo hicho huenda kikamuweka katika wakati mgumu, licha ya kwamba soka ndivyo lilivyo, lakini mashabiki wa Yanga waliokuwa wakiamini wangeshinda gemu hiyo wanaoenekana hawaamini kama wamefungwa na mtani wao licha ya klabu yao kuzoa poiinti nyingi za promosheni ya Nani Mtani Jembe na kuondoka na Sh. Milioni 98 wakati Simba ikitwaa ubingwa na Sh., Mi. 1.6 tu.

No comments:

Post a Comment