STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 21, 2013

Kila la heri Tanzanite kwa Madiba

WAKATI macho na masikio ya mashabiki wa soka leo wanaelekezwa kwenye pambano la soka la Simba na Yanga, wawakilishi wa Tanzania katika kuwania tiketi ya kushiriki Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake U20 Tanzanite wapo Afrika Kusini kujaribu kuutafuna mfupa uliowashinda wiki mbili zilizopita.
Tanzanite watawakabilia wenyeji wao, katika pambano la marudiano ya raundi ya pili ya michuano hiyo baada ya kuchezea kichapo cha mabao 4-1 nyumbani.
Kocha wa timu hiyo Rogatian Kaijage amewapa matumaini Watanzania kwamba watapigana kiume dhidi ya wenyeji wao, ingawa hatarajii miujiza yoyote katika pambano hilo.
Tanzanite iliyowang'oa Msumbiji kwa kipigo cha mabao 15-1 katika mechi zilizopita kama itafanikiwa kuitoa Afrika kusini itaumana na mshindi kati ya Nigeria au Tunisia katika hatua ya mwisho ya kuwania nafasi mbili za kwenda Canada kwenye fainali za dunia mwakani.
Kila la heri kwa wawakilishi wetu hao, hatya kama akili zetu zitakuwa kwenye pambano ma Nani Mtani Jembe linalochezwa jioni hii uwanja wa Taifa, kati ya Simba na Yanga.

No comments:

Post a Comment