STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 21, 2013

Liverpool yaiengua Arsenal kileleni, Suarez aendelea kuua EPL

Liverpool striker Luis Suarez (right) volleys in against Cardiff at Anfield
Suarez akitupia kambani moja ya mabo yake muda mfupi uliopita wakiizamisha Cardiff City

VIJOGOO vya Anfield, Liverpool imekalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu ya England baada ya kuinyuka Cardiff City kwa mabao 3-1 na kuiengua Arsenal ambayo yenyewe itashuka dimbani Jumatatu kuumana na Chelsea.
Mabao mawili ya Luis Suarez katika dakika ya 25 na 45 kwa pasi za Henderson na goli jingine ya Raheem Sterling zilitosha kuwapeleka Liver kileleni kwa kufikisha pointi 36, moja zaidi ya ilizonazo Arsenal.
Bao la kuftia machozi la wageni lilifungwa na Jordon Mutch katia dakika ya58 kipindi cha pili ambalo halikufanya Liverpool kutetereka.
Mabao mawili aliyofungwa Suarez ambaye mechi ya pili sasa anacheza kama nahodha baada ya Steven Gerrard na msaidizi wake kuwa majeruhi yamemfanya afikishe jumla ya mabao 19 katika orodha ya wafungaji wa ligi hiyo akiendelea kuongoza kileleni.
Jioni hii kuna mechi kadhaa zinachezwa ikiwamo ile ya Manchester City kuumana na Fulham ugenini na Machester United kuwakaribisha West Ham United.

No comments:

Post a Comment