STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 26, 2013

Majaribio tiketi za Electroniki saa 10 leo

MECHI ya kujaribu matumizi ya tiketi za elektroniki kati ya Azam na Ruvu Shooting inachezwa leo (Desemba 26 mwaka huu) saa 10 kamili jioni Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Viingilio katika mechi hiyo ya majaribio ni sh. 1,000 na sh. 2,000 ambapo tiketi zinapatikana kupitia M-Pesa na mawakala wa CRDB Fahari Huduma. Tiketi zitaendelea kuuzwa hadi kitakapoanza kipindi cha pili.
Mawakala 18 wa Fahari Huduma wanaouza tiketi hizo ni ABC Computer- Mtaa wa Samora, Abraham Anangisye Mwampetele- Maji Matitu, Apex Security Services- Mtaa wa Mibega, Kinyerezi, Athuman Fakhi Adam- Kongowe Mbagala, Fedha Investment Limited- Pamba Road na Fuya Godwin Kimbita- Tegeta Block.
Ghomme Health & Education Limited-Bahari Beach, Herman Arbogast Tarimo- Kigamboni, K- Finance Limited- Shekilango, Sinza, Koli Finance Limited- Mtaa wa Samora, LB Pharmacy- Mtoni Kijichi, Lista Phares Barnabas- Tabata Segerea na Maly Investment Company Limited.
Wengine ni Micu Enterprises- Mtaa wa Congo, Kariakoo, S&D Collection Company Limited- Mikocheni, Shoppers Plaza, Therry Investment Limited- Tegeta Kibaoni, TSHS Distributors Limited- Mtoni kwa Aziz Ali na Wemerick Independent Vehicle- Mtaa wa Boko, .
Mechi nyingine ya majaribio itakuwa kati ya Ashanti United na JKT Ruvu ambayo itachezwa Januari Mosi mwakani kwenye uwanja huo huo.

No comments:

Post a Comment