STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 7, 2013

Man Utd bado gonjwa, Chelsea hoi, Liverpool haishikiki England

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/71601000/jpg/_71601162_71601161.jpg
Hawaamini macho yao kama wanaweza kulowa nyumbani mara mbili mfululizo
Cabaye akishangilia bao lililoizamisha Man Utd
Tough task: West Ham's defence could not keep Suarez in check for the full 90 minutes
Suarez akichuana na mchezaji wa West Ham ambapo Liverpool imeshinda mabao 4-1, Suarez akifunga moja na jingine kumbabatiza beki wa wapinzani wao.

Mmorocco Ossuman Assaidi akishangilia bao lake lililoizamisha Chelsea 'jioni'

MABINGWA watetezi wa Ligi ya England, Manchester United imeendelea kuwa 'urojo' baada ya jioni jii kupigwa tena bao 1-0 na Newcastle United ikiwa nyumbani Old Trafford, huku Chelsea ya Jose Mourinho wakionja kipigo wakiwa ugenini dhidi ya Stoke City.
Manchester inayonolewa na David Moyes ilikumba na kipigio hicho cha pili mfululizo baada ya majuzi kunyukwa kama hivcyo na Everton na kuzidi kuwapa wakatiu mgumu mashabiki wa timu hiyo ambao waliozoea kushinda enzi za Sir Alex Ferguson.
Bao lililizamisha Mashetani Wekundu, lilifungwa na Yohan Cabaye dakika ya 61 na kumfanya Moyes kukuna kichwa namna ya kuepukana na vipigo mfululizo ambavyo zimeifanya timu yake kusalia na pointi zake 22 na kung'ang'ania nafasi ya 9.
Katika mechi nyingine, Chelsea ilijikuta ikinyolewa mabao 3-2 na Stoke City, huku Liverpool ikiendelea kufanya mauaji ya shalubela baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-1 dhidi ya West Ham United kwenye uwanja wa Anfield.
Licha ya kutangulia kupata bao kupitia kwa Andre Schürrle katika dakika ya 9, Chelsea ilishindwa kuendeleza ubabe baada ya Peter Crouch kulisawazisha dakikia tatu kabla ya mapumziko na Stephen Ireland kuongeza la pili.
Schurrle alisawazisha bao hilo dakika ya 53 ikiwa dakika tatu kabla ya wenyeji kupata bao lake na kuonekana kama matokeo yangeisha kwa sare ya 2-2 kabla ya Oussuma Assaidi kufunga bao dakika ya 90 na kuzimisha vijana wa darajani.
Liverpool waliyopata ushindi mnono wa mabao 5-1 juzi dhidi ya Norwich City iliendelea kufanya mauaji kwa kuicharaza West Ham mabao 4-1 yaliyowekwa kimiani na Guy Demel, Mamadou Sakho, kabla ya Martin Skrtel kujifunga na kuwapa wageni bao la kufutia machozi.
Hata hivyo  Luis Suarez alifunga bao la tatu na  wageni nao wakajifunga kupitia kwa Obrein na kuifanya Liverpool kuijongelea Arsenal kileleni kwa sasa.
Katika mechi nyingine, Cardiff City ikiwa ugenini ilikumbana na kipigo cha mabao 2-0 toka kwa Crystal Palace, huku Norwich City ikapata ushindi ugenini dhidi ya wenyeji wao West Brom wa mabao 2-0 na timu za Manchester City ililazimisha sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Southampton.
Kwa sasa timu za Sunderland na Tottenham Hotspur zinaendelea kuonyeshana kazi, Spurs wakiwa ugenini.

No comments:

Post a Comment