STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 7, 2013

Bayern Munich yazidi kutakata Ujerumani, Ribery arejea na mawili


http://cache.images.globalsportsmedia.com/news/soccer/2013/12/5/402988header.jpg

MABINGWA watetezi wa Bundesliga, Bayern Munich wameendeleza rekodi yao ya kutopotezaq mchezo baada ya jioni hii kutoa kipigo cha 'mbwa mwizi' cha mabao 7-0 dhidi ya Werder Bremen na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.
Mabavarian hao ambao pia ni mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, walijipatia mabao yake kupitia kwa  beki wa wenyeji Bremen, Assani Lukimya kujifunga kabla ya Daniel Van Buyten, Frank Ribery aliyefunga mara mbili, Mario Mandzukic, Thomas Muller na Mario Gotze.
Katika mechi nyingine za ligi ambayo Bayern wanaendelea kuongoza wakiwa na pointi 41, saba zaidi ya timu inayopifuata katika nafasi ya pili, jana Nurnberg ilizamishwa sare ya 1-1 na Mainz 05, Borussia Monchengladbach kuilaza Schalke 04 kwa mabao 2-1, Stuttgart kuilamba Hannover 96  mabao 4-2, huku  Hamburger SV ikilala 1-0 nyumbani mbele ya Augsburg nayo Eintracht Frankfurt kukubali kipigo nyumbani dhidi ya Hoffenheim iliyoshinda mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment