STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 7, 2013

PSG yazinduka na kufanya 'mauaji' Ufaransa

Zlatan Ibrahimovic
Kitu! Zlatan Ibrahimovic akifunga moja ya mabao yake jioni hii katika ligi ya Ufaransa

BAADA ya 'kutenguliwa' udhu majuzi na timu ya Evian TG, mabingwa watetezi wa Ufaransa, PSG jioni hii imemaliza hasira zake kwa Sochaux kwa kuishindilia mabao 5-0 katika mfululizo wa mechi za Ligi ya nchi hiyo.
PSG ilipata ushindi huo ikiwa uwanja wake wa nyumbani kwa mabao ya Thiago Silva aliyefunga dakika ya  14 akimalizia kazi ya Zlatan Ibrahimovic kabla ya Ezequeil Lavezzi kufunga bao la pili dakika ya 47 na Edinson Cavani kutupia bao la tatu dakika ya 62 akimaliza pasi murua ya Ibrahimovic.
Zlatan aliongeza mabao mengine mawili katika dakika ya 87 na dakika ya 90+1 na kuifanya PSG iendelea kukalia kiti cha uongozi cha ligi hiyo ikiwa na pointi 40.

No comments:

Post a Comment