STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 7, 2013

Mario Balotelli aiokoa Milan ugenini, Juve dah!

 http://cdn.bleacherreport.net/images_root/slides/photos/003/451/372/hi-res-452749825-mario-balotelli-of-milan-celebrates-his-teams-second_crop_650x440.jpg?1385904879
SUPER Mario Balotelli aliyenukuliwa kwamba ataacha utukutu wake, ameifungia timu yake ya AC Milan mabao mawili na kupata sare ya mabao 2-2 ugenini dhidi ya Livorno katika mfululizo wa Ligi ya Italia (Seria A) muda mfupi uliopita.
Balotelli alianza kwa kuwashtua wenyeji kwa kufunga bao la kuongoza dakika ya saba tu ya mchezo huo kwa kujunganisha krosi pasi ya Kaka kabla ya wenyeji kusawazisha kupitia kwa Luca Siligardi dakika ya 26 na kwenda mapumziko timu hizi zikiwa nguvu sawa ya kufungana 1-1.
Kipindi cha pili wenyeji walijipatia bao la pili lililotupiwa kambani na Paulinho katika dakika ya 58 kabla ya Balotelli kusawazisha dakika saba kabla ya pambano hilo kumalizika na kuipa pointi moja muhimu Milan ambayo msimu hii imekuwa na wakati mgumu Seria A.
katika mechi nyingine iliyochezwa jana, vinara na watetezi wa ligi hiyo Juventus ilipata ushindi muhimu wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Bologna kwa mabao ya Arturo  Vidal na  Giorgio Chiellini na kufikisha pointi 40 na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo huo.

No comments:

Post a Comment